domingo, 8 de octubre de 2017

Tamko la ACT Wazalendo baada ya JPM kuteua Katibu mpya wa Bunge



Magufuli jana October 7, 2017 alifanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri ambapo zimeongezwa Wizara mbili kutoka 19 za awali hadi 21 huku pia idadi ya Naibu Mawaziri ikipanda kutoka 16 hadi 21 ambapo mbali na mabadiliko hayo ya Baraza hilo, Rais pia alifanya uteuzi wa Katibu wa Bunge.
Kutokana na uteuzi huo, kumekuwa na mitazamo na maoni mbalimbali kutoka kwa watu binafsi, wasomi na vyama vya siasa na miongoni mwao ni Chama cha ACT Wazalendo ambao baada ya uteuzi wa Katibu wa Bunge, kimetoa tamko kupitia kwa
Katibu, Itikadi, Mawasialiano na Uenezi, Ado Shaibu.

Jana, Oktoba 7, 2017, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amefanya teuzi mbalimbali ikiwemo uteuzi wa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
ACT Wazalendo tunasikitika kusema Kwamba kama ilivyo desturi, Rais ameamua kuyaweka pembeni matakwa ya Sheria yanayoongoza mchakato wa uteuzi wa Katibu wa Bunge na kuamua kujichagulia apendavyo.
Kutokana na unyeti wa nafasi ya Katibu wa Bunge, na kwa minajili ya kuweka ‘check and balance’ pamoja na kulinda uhuru wa Bunge, kwenye mchakato wa uteuzi wa nafasi husika, sheria imeweka utaratibu wa kufuatwa kwenye uteuzi wa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hivyo basi, mbali na Rais kuwa na mamlaka ya kumteua Katibu wa Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 87 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anapaswa kuzingatia utaratibu uliowekwa na Sheria ya Utawala wa Bunge – The National Assembly (Admintration Act), 2015. Kwa mujibu wa Kifungu cha 7(3) cha Sheria hiyo, Rais atateua jina moja kutoka miongoni mwa majina matatu yaliyopendekezwa na Tume ya Huduma za Bunge.
Jambo hili sio la hiyari. Ni sharti la lazima la sheria ambalo Rais analazimika kulifuata. Ndio maana kifungu husika kinasema “The Commision shall recommend three names” (Tume ni LAZIMA ipendekeze majina matatu).
Wajumbe wa Tume ya Huduma za Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 12(2) cha Sheria ya Utawala wa Bunge ni wafuatao:
1. Ndg. Job Ndugai, Spika wa Bunge
2. Ndg. Tulia Akson, Naibu Spika wa Bunge
3. Ndugu Jenister Mhagama – Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu – Bunge
4. Ndg. Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni
5. Ndg. Magdalena Sakaya – Kamishna wa Bunge (CUF)
6. Ndg. Peter Msigwa – Kamishna wa Bunge (Chadema)
7. Ndg. Salim Hassan Abdullah Turky – (Kamishna wa Bunge – CCM)
8. Ndg. George Masaju
9. Ndg. Mary Chatanda (Kamishna wa Bunge – CCM)
10. Ndg. Kangi Lugola-(Kamishna wa Bunge-CCM)
11. Ndg. Mussa Hassan Zungu-(Kamishna wa Bunge-CCM)
Kwa taarifa tulizonazo, hakuna kikao chochote cha Tume ya Bunge kilichoketi na kupendekeza majina kwa Rais kwa ajili ya uteuzi wa Katibu wa Bunge. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wajumbe wote wa Tume ya Huduma za Bunge waliohojiwa na vyombo vya habari wamethibitisha pia kutofanyika kwa kikao hicho.
Hitimisho:
1. ACT Wazalendo tunaona kuwa uteuzi huu si tu ni mwendelezo wa Rais kufanya maamuzi bila kuzingatia sheria za nchi bali ni ushahidi mwingine wa wazi wa kudharau mhimili wa Bunge.
2. Ni matumaini yetu kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano na watu wote wanaopenda uhuru na uimara wa Bunge watasimama imara kuupinga uteuzi huu ambao ni kinyume na sheria.
3. Kama Rais hatatengua uteuzi huu na kufuata utaratibu uliowekwa na Sheria za nchi, ACT Wazalendo kitalifikisha suala hili Mahakamani ili kupata ufafanuzi wa mahakama.
4. Ni wakati muafaka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ndiye mwenye dhamana ya kuishauri serikali kwenye masuala ya kisheria kuwajibika. ACT Wazalendo tunaamini suala hili na vitendo vingine vya huko nyuma vimetokea kwa sababu ya moja ya sababu mbili. Inawezekana Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwa woga au uzembe, hamshauri Rais ipasavyo au Rais hafuati ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Katika yote mawili, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kama anataka kulinda heshima yake binafsi na ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hana budi KUJIUZULU.

RAISI ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI NA WACHACHE WANG'OKA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Mgufuli ametangaza baraza lake dogo jipya la mawaziri lenye wizara 18, huku akiwabakiza mawaziri wa zamani 7 na kuingiza sura mpya katika baraza hilo litakalokuwa na jumla ya mawaziri na manaibu waziri 34 tu.
Aidha, katika baraza hilo Rais Dk. Magufuli ameacha wazi nafasi za uwaziri katika wizara nne ambazo ni Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Ujenzi pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambazo amesema bado hajapata watu wa kuwakabidhi majukumu ya uwaziri.
Dk. Magufuli amesema serikali yake imepunguza bazara la mawaziri ili mawaziri walioteuliwa wakafanye kazi, na kusisitiza hakutakuwa na semina elekezi ambapo ameagiza fedha zaidi ya shilingi bilioni 2 zilizotengwa kwa semina hiyo kuchukuliwa na kutumika katika shughuli nyingine.
Aidha, Dk. Magufuli akatuma salamu kwa mawaziri aliowateuwa katika baraza lake ambao wanapenda kufanya sherehe wajue wamepewa kazi ngumu na iwapo watafanya sherehe hizo wajiandae na kufanya sherehe pia wakati watakapotimuliwa kazi.
BARAZA LA MAWAZIRI
Wizara ya Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora.
Mawaziri - George Simbachawene na Angella Kairuki
Naibu Waziri - Sumeilam Jafo. Naibu.
Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, Muungano na Mazingira
Waziri - January Makamba
Naibu Waziri – Luhaga Jerrson Mpina
Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu
Waziri - Jenista Muhagama
MaNaibu – Dkt. Possy Abdallah na Anthony Mavunde.
Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
Waziri - Mwigulu Nchemba
Naibu Waziri - William Ole Nasha
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Waziri Bado hajapatikana.
Naibu Waziri – Inj. Edwin Ambandusi Ngonyani
Wizara ya Fedha na Mipango
Waziri Bado hajapatikana.
Naibu Waziri - Ashantu Kizachi
Wizara ya Nishati na Madini
Waziri - Prof. Mwigalumi Muhongo.
Naibu Waziri - Medalled Karemaligo.
Wizara ya Katiba na Sheria,
Waziri - Harrison Mwakyembe
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.
Waziri - Dk. Augustino Mahiga
Naibu Waziri – Dkt. Susan Kolimba.
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Waziri - Dk. Hussein Mwinyi
Wizara ya Mambo ya Ndani
Waziri - Charles Kitwanga.
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Waziri - William Lukuvi
Naibu Waziri - Angelina Mabula
Wizara ya Maliasili na Utalii
Waziri Bado hajapatikana.
Naibu Waziri– Inj. Ramol Makani
Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
Waziri Charles Mwijage.
Wizara ya Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi.
Waziri Bado hajapatikana.
Naibu Waziri – Inj. Stella Manyanya
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Waziri - Ummy Mwalim
Naibu Waziri – Dkt. Hamis Kigwangala
Wizara ya Habari, Utamadu, Wasanii na Michezo
Waziri - Nape Nnauye
Naibu Waziri - Anastasia Wambura.
Wizara ya Maji na Umwagiliaji
Waziri – Prof. Makame Mbarawa
Naibu Waziri– Inj. Isack Kamwela

CCM ZANZIBAR YAIFARIJI FAMILIA ILIYOPATA AJALI YA MOTO NA KUFARIKI WATU WANNE.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi akiwafariji ndugu na jamaa wa marehemu wa familia iliyopata msiba huo katika k...