lunes, 9 de octubre de 2017

Jela kwa kumshika mwanaume mwenzie kiuno

Mwanaume mmoja ajulikanaye kama Jamie Harron ambaye ni raia wa Scotland anakabiliwa na kifungo cha miaka 3 mjini Dubai baada ya kugusa kiuno cha mwanaume mwingine wakiwa bar.
Mwanaume huyo ambaye ana umri wa miaka 27, alikamatwa kwa kile kilichosemwa kuwa ameonesha tabia mbaya hadharani kwa kumshika mwanaume mwenzie kiuno jambo ambalo halikubaliki kabisa kwenye jamii hiyo.
Kwa mujibu wa Jamie akiwa kwenye bar iitwayo Rock Bottom alikuwa anajaribu kuzuia kumwaga kinywaji chake kwenye baa hiyo iliyokuwa imejaa watu, kwa kuweka mikono mbele na kujikuta akimgusa mwanaume huyo kimakosa kwenye kiuno ikiwa anaepuka kumgonga.

Mradi wa Kuwezesha Umilikishaji Ardhi ( LTSP ) Wapokelewa na Wananchi Wilayani KILOMBERO



Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga akitoa Mada kuhusu Ujenzi na Ukarabati wa Masjala za Ardhi katika Kijiji cha Sululu Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro,Uhamasishaji huu unaendelea unafanywa pia katika Vijiji Vingine unafanywa na Wizara ya Ardhi, kupitia Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi (LAND TENURE SUPPORT PROGRAME - LTSP),Programu hii inafanya utekelezaji wake ndani ya Miaka mitatu katika Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga, Mkoano Morogoro.
Baadhi Wananchi ambao ni Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Sululu wakiangalia ramani ya masjala ya Ardhi, inayotakiwa kujengwa katika kijiji hicho,kupitia Programu ya kuwezesha Umilikishaji Ardhi,(LAND TENURE SUPPORT PROGRAME - LTSP), mradi ambao upo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mmoja wa Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Sululu Wilayani Kilombero, akichangia Mada iliyowasilishwa na Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga, iliyokuwa ikihamasisha Ujenzi wa Masjala ya kijiji,ambapo pamoja na mambo mengine,itatumika kuhifadhi hatimiliki za kimila (CCROs),ambazo zitatolewa baada ya Programu ya kupima Ardhi za Vijiji katika wilaya za Mfano za Malinyi, Kilombero na Ulanga kukamilika.
Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga katika Meza Kuu akiwa pamoja na watumishi wengine kutoka Wizara ya Ardhi pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Sululu ( kushoto) na Mtendaji Kata kushoto kwake,akiandika kitu kwenye karatasi zake ili kuweka kumbukumbu sawa,wakati wa mkutano wa kuhamasisha Ujenzi wa masjala ya Kijiji,kupitia Programu ya kuwezesha umilikishaji Ardhi (LAND TENURE SUPPORT PROGRAME) - LTSP ),mradi ambao upo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi.
Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga ( watatu kushoto ) waliosimama akiwa kwenye Picha ya Pamoja na Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Sululu Wilayani Kilombero, Morogoro.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Sululu, akifungua mkutano wa Kuhamasisha Ujenzi wa Masjala za Ardhi Wilayani Kilombero, Kupitia Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi ( LAND TENURE SUPPORT PROGRAME - LTSP ) mradi ambao unasimamiwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga,kupitia Programu ya LTSP chini ya Wizara ya Ardhi inayotekelezwa katika Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga Mkoani Morogoro, akitoa Semina elekezi Juu ya Mradi huo, wenye lengo la kupima mipaka ya vijiji na kutoa hatimiliki pamoja na kuhamasisha Ujenzi wa masjala za Ardhi kwenye Vijiji.
Sehemu ya Umati wa Wananchi wa Kijiji cha Sululu Wilayani Kilombero wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Kuongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga,kuhusu umuhimu wa ujenzi wa Masjala ya Kijiji,kupitia Programu ya kuwezesha Umilikishaji Ardhi(LANDA TENURE SUPPORT PROGRAME),Mradi unaosimamiwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Kaimu kamishna wa Ardhi nchini Bi Mary Makondo, akifafanua Jambo kwa Waandishi wa habari wilayani Ulanga, kuhusu mradi wa Kuwezesha Umilikishaji Ardhi katika Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga, ikiwemo upimaji wa Mipaka ya Vijiji na Utoaji wa hatimiliki kwa Vijiji 37 vya Wilaya hizo.
Mratibu wa Mradi wa Kuwezesha Umilikishaji Ardhi, ambao upo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ndugu Godfrey Machabe akizungumza Jambo Mbele ya Kaimu Kamishna wa Ardhi, Bi Mary Makondo muda mfupi Baada ya kumalizika kwa Kikao na Watendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro kuhusu utekelezwaji wa Mradi wa LTSP.
Picha zote na Hannah Mwandoloma

PROF TIBAIJUKA! Kaeleza changamoto baada ya Rugemalira kuwa matatizoni



Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka amebainisha namna wanavyokabiliwa na changamoto katika uendeshaji wa Shule ya Wasichana ya Kajumulo Alexander iliyopo Bukoba baada ya mmoja wa wafadhili wa shule hiyo James Rugemalira kuwa matatizoni.
Prof. Tibaijuka amesema hakuanzisha shule kibiashara badala yake alijitoa kwa ajili ya kuwasaidia wasichana na kuwainua kielimu ndio maana anajitoa kwa kile alichonacho kuwasaidia watoto hao kwa kushirikiana na wafadhili wake huku akisema kuwa kwa sasa amebaki mwenyewe katika kuchangia baada ya mfadhili wake mkubwa James Rugemalira kushikiliwa na Polisi.

CCM ZANZIBAR YAIFARIJI FAMILIA ILIYOPATA AJALI YA MOTO NA KUFARIKI WATU WANNE.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi akiwafariji ndugu na jamaa wa marehemu wa familia iliyopata msiba huo katika k...