lunes, 9 de octubre de 2017

Jela kwa kumshika mwanaume mwenzie kiuno

Mwanaume mmoja ajulikanaye kama Jamie Harron ambaye ni raia wa Scotland anakabiliwa na kifungo cha miaka 3 mjini Dubai baada ya kugusa kiuno cha mwanaume mwingine wakiwa bar.
Mwanaume huyo ambaye ana umri wa miaka 27, alikamatwa kwa kile kilichosemwa kuwa ameonesha tabia mbaya hadharani kwa kumshika mwanaume mwenzie kiuno jambo ambalo halikubaliki kabisa kwenye jamii hiyo.
Kwa mujibu wa Jamie akiwa kwenye bar iitwayo Rock Bottom alikuwa anajaribu kuzuia kumwaga kinywaji chake kwenye baa hiyo iliyokuwa imejaa watu, kwa kuweka mikono mbele na kujikuta akimgusa mwanaume huyo kimakosa kwenye kiuno ikiwa anaepuka kumgonga.

0 comentarios:

Publicar un comentario

CCM ZANZIBAR YAIFARIJI FAMILIA ILIYOPATA AJALI YA MOTO NA KUFARIKI WATU WANNE.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi akiwafariji ndugu na jamaa wa marehemu wa familia iliyopata msiba huo katika k...