sábado, 7 de octubre de 2017

MSIBA HARUSINI: Bibi harusi kafariki saa 11 baada ya kuolewa kisa?

Kwenye Leo Tena ya Clouds FM leo August 2, 2017 Mtangazaji Geah Habib ameifikisha Hekaheka iliyotokea Mtoni Kijichi DSM ambako nyumba ya Harusi iligeuka kilioni baada ya mwanamke kuolewa na kufariki saa 11 baadaye.


 Pichani ni bibi harusi
Tukio hilo linatajwa kutokuwa la kawaida baada ya ndoa kufungwa saa Kumi Alasiri na Bibi Harusi kufariki saa Kumi na Moja Alfajiri huku ikidaiwa kuwa alikuwa na ujauzito wa Miezi Sita.
Inaelezwa kuwa siku ya tukio Bwana Harusi aliwapigia simu ndugu wa mkewe kuwapa taarifa ya kuumwa ghafla mkewe ambapo alikuwa analalamika kuumwa tumbo na kumkimbiza Hospitali usiku huo ambako baadaye alifariki.

0 comentarios:

Publicar un comentario

CCM ZANZIBAR YAIFARIJI FAMILIA ILIYOPATA AJALI YA MOTO NA KUFARIKI WATU WANNE.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi akiwafariji ndugu na jamaa wa marehemu wa familia iliyopata msiba huo katika k...